Psalms 8

Utukufu Wa Mungu Na Heshima Ya Mwanadamu

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Daudi.

1 aEe Bwana, Bwana wetu,
tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

Umeuweka utukufu wako
juu ya mbingu.
2 bMidomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao
umeamuru sifa,
kwa sababu ya watesi wako,
kumnyamazisha adui na mlipiza kisasi.

3 cNikiziangalia mbingu zako,
kazi ya vidole vyako,
mwezi na nyota,
ulizoziratibisha,
4 dmwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria,
binadamu ni nani hata unamjali?
5 eUmemfanya chini kidogo kuliko viumbe wa mbinguni,
ukamvika taji ya utukufu na heshima.

6 fUmemfanya mtawala juu ya kazi za mikono yako;
umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.
7 gMifugo na makundi yote pia,
naam, na wanyama wa kondeni,
8 hndege wa angani na samaki wa baharini,
naam, kila kiogeleacho katika njia za bahari.

9 iEe Bwana, Bwana wetu,
tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!
Copyright information for SwhNEN